Social Icons

Saturday, May 4, 2013

TAARIFA YA IDARA YA MAWASILIANO UDOM 2011/1013





                            KANISA LA WAADVENTISTA WASABATO

                                      
















  TANZANIA HIGHER LEARNING INSTITUTION OF SEVENTH DAY ADVENTIST                                    STUDENT ORGANISATION    (THISDASO) 
                                            IDARA YA MAWASILIANO
                                        CHUO KIKUU CHA DODOMA
            EMAIL: thisdasoudom@gmail.com
             BLOGSPOT: thisdasoudom.blogspot.com

                                    TAAARIFA YA UTENDAJI KAZI
                               DECEMBER 25, 2011  -  APRIL 4. 2013

VIONGOZI
1.      ISAAC DOTTO                                              MKUU  (SOCIAL SCIENCE)
2.      RAFAEL MWAMBENJA                              SOCIAL SCIENCE
3.      ALLY KIBONA                                              HUMANITIES
4.      MAPENZI JAMES                                           EDUCATION
5.      KAZIMOTO TOBIAS                                     INFORMATICS
6.      MTATILO EZEKIEL                                      MEDICINE





                                                            YALIYOMO
1.      UTANGULIZI
      2.   SHUKRANI
      3.    MALENGO
     4.     MAFANIKIO
     5.    MAPATO NA MATUMIZI
     6.    CHANGAMOTO
     7.    MAONI
     8.    MWISHO


UTANGULIZI
Idara ya mawasiliano inapenda kuwaletea taarifa ya utendaji kazi tangu ilipokabiziwa december 2011 hadi leo April 4, 2013.


1.      SHUKRANI
Tunapenda kumshukuru Mungu awali ya yote kwa  uweza wake kwa kutuweka salama kuanzia kipindi tulipoanza kazi hadi hivi leo. Pia tunapenda kuushukuru uongozi wa THISDASO-UDOM chini ya mwenyeketi wake Abayo Asubuhi, Daniel Karangi pamoja na Gerald Asubiswe, makatibu wote na idara zote za THISDASO chuo kikuu Dodoma. Hatuwezi pia kuwasahau wanachama wenzetu kwa ushirikiano waliotupatia katika utendaji kazi katika idara hii nyeti ya mawasiliano wote kwa pamoja tunawashukuru sana na Mungu awabariki na kuwazidishia zaidi.

 

2.      MALENGO
Tangu kuanza kwa kipindi chetu cha uongozi idara imekuwa na malengo mbalimbali katika makundi mawali, yaani malengo ya muda mfupi nay ale ya muda mrefu.

2.1  MALENGO YA MUDA MFUPI
Haya ni malengo ambayo idara imekuwa ikiyatendea kazi kwa ukaribu zaidi kuhakikisha idara inaendelea vizuri katika utendaji wake. Malengo hayo ni kama ifuatavyo;

(i). idara ilidhamiria kuongeza vifaa vya mawasiliano ambavyo vimekuwa vikitumika katika ibada zetu. Baadhi ya vifaa idara ilivyodhamilia kuwa navyo ni kama ifuatavyo;

·         Hornspeaker 2   @tsh 150, 00
·         Keyboard organ PSR 7000          1,800,000
·         Wireless microphone   1 set    @ths 200,000
·         Flash 1, 4GB                          @ths 20,000
·         Modem 1 (multipurpose)         @tsh 50,000
·         Microphone cover 10                @tsh 1000
·         Headphone 1                             @ tsh 30,000
     (ii).  Idara ilidhamilia kuendelea kutafuta chumba cha kuhifadhia vyombo vya                                           mawasiliano kutokana na changamoto zilizokuwepo mahali pa kuhifadhia                                       vyombo.
     (iii). Idara pia ilidhamiria kulihusisha kanisa katika operation ya generator kwa kununua            mafuta ya kila wiki ya ibada pindi panapotokea tatizo la umeme.
     (iv). Idara ilidhamiria kuendelea kuiboresha blogspot ya chama kwa kuweka taarifa                  mbalimbali na masomo mbalimbali ambayo ingesaidia kufikisha taarifa kwa wanachama   katika vitivyo vyetu.
     (v). Idara ilidhamiria kubadilisha code za usajili wa vyombo awali ikiwa ni                    T.UDOM/PA/CMPT/01 na kupendekezwa kuwa THISDASO/UDOM/PA/MIC/01.
    (vi). Idara ilidhamiria kuvifanyia mainteinance vyombo vya mawasiliano kila mara kuvilinda                 katika ubora wake kwa manufaa ya muda mrefu. Tulitarajia kuwa na Tsh 1,000,000 kwa ajili ya maintenance hii.
   (vii). Idara illiahidi kuonyesha ushirikiano kwa uongozi wote na idara mbalimbali katika                         utendaji wa kazi ya Bwana. Aidha idara kwa kushirikiana na uongozi pamoja na                        wanachama ilikuwa ikitoa vyombo maeneo nje na chuo chetu pindi vyombo vilipokuwa                       vikiombwa kwa shughuli mbalimbali.
   (viii). Idara ilidhamiria kuwa na pesa ya uchakavu TSH. 20,000 pindi vyombo vilipokuwa                      vikiombwa kutumika nje na eneo letu.
   (ix).  Idara ilidhamilia kujenga uhusiano mzuri kwa wanachama kwa kushirikiana na wakuu wa program coordinators na wakuu wa kiroho katika kendesha shughuli mbalimbali za              kiroho chuoni kwetu.
  (x). Idara ilidhamiria kuandaa DVD za matukio mbalimbali za ibada zetu pamoja na mikutano                mbalimbali ya injili iliyokuwa ikifanyika katika uhusika wetu. Kwa mfano mikutano ya                        effort na uzinduzi wa  kwaya  zetu n.k.
(xi).  Idara ilidhamiria kutohusika kuburn nyimbo au album za kwayya mbalimbali zilizomo                       katika maktaba yetu ya mawasiliano mbali idara ilidhamiria kutoa masomo na                   mafundisho yoyote pale wanachama walipoyahitaji kwa kujifuanza zaidi.
(xii).  Idara ilidhamiria kuendelea kushughulikia tatizo la usafiri hasa siku za ibada licha ya                        changamoto mbalimbali zinazojitokeza.
(xiii). Idara ilidhamiria kuendelea kutoa taarifa za utendaji kazi wake katika kipindi hiki cha                      uongozi hadi mwisho wa uongozi pia.

            MALENGO YA MUDA MREFU.
·         Idara ilidhamiria kuwa na harakati za kuwa na gari la chama kwa ikiwa ni moja ya miradi ya chama. Hivyo kamati maalum itaundwa kwa ajili ya kushughulikia suala hili ni vipi tutaweza kunua hili gari pamoja na uedeshaji wake.
·         Idara ilidhamiria kununua photocopy machine itakayo rahisisha upatikanaji wa nakala mbalimbali.
·         Idara pia ilidhamiria kuendelea kutoa mafunzo mbalimbali ya utumiaji wa vifaa vya mawasiliano kwa wanachama wake.
·         Idara pia ilitarajia kuongeza vifaa vingine vya mawasiliano kama vile video camera, external disk, stendi za microphone na boxspeaker moja.

3.      MAFANIKIO
Tunamshukuru Mungu katika malengo tuliyokuwa nayo katika kuyatekeleza katika kipindi hiki cha uongozi. Idara imeweza kufanikiwa kutekeleza mambo yafuatayo;
1.      Idara imeweza kufanikiwa kuongeza baadhi ya vifaa kama vile cable 3 za microphone @ 20,000, sponge 5 za microphone @2,000 na sanduku kwa alili ya kutunzia laptop pamoja na projector kwa gharama ya Tsh 60,000.
2.      Idara pia imefanikiwa kuweza kupata chumba cha kuhifadhia vyombo vya mawasiliano humanities kwa gharama ya Tsh 50,000 lakini upande wa COED bado tunachangamoto ya chumba kwa ajili ya kuhifadhiwa vyombo vyetu vya mawasiliano ila tunaendelea kufuatilia suala hilo.
3.      Idara imefanikiwa katika kulihusisha kanisa katika kulihudumia kundi la UDOM na tumekuwa tukiendelea kupata mafuta  kwa ajili ya generator pale tulipokuwa na uhitaji huo.
4.      Idara imeendelea kushughulikia blogspot ya chama kwa kuweka taarifa mbalimbali zinazohusiana na chama chetu ili kurahisisha upatikanaji wa taarifa mbalimbali.
5.      Idara imefanikiwa kuonyesha ushirikiano na viongozi wengine katika idara tofauti tofauti katika kufanya kazi mbalimbali katika idara husika.
6.      Idara imefanikiwa kuwa na pesa za uchakavu kiasi cha Tsh 20,000 pindi vyombo vilipokuwa vikitumiaka nje ya eneo letu kama vile kwenye harusi  na sehemu nyinginezo.
7.      Idara imefanikiwa kuwa na uhusiano mzuri na wanachama kwa kushirikiana na program coordinators, na wakuu wa mambo ya kiroho katika kuendesha shughuli mbalimbali za kiroho katika chuo chetu.
8.      Idara pia imefanikiwa kutengeneza DVD yenye matukio mbalimbali kama vile effort zinazofanyika na mikutano ya ibada katika chuo chetu. DVD hizi zinapatikana katika maktaba ya mawasiliano japo hazikutangazwa lasmi kuanza kuuzwa kwa wanachama kwa gharama ya Tsh 1500.
9.      Idara imefanikiwa katika kujihusisha kuburn DVD za nyimbo za album za kwaya au vikundi mbalimbali kwa ajili ya kulinda kazi ya watu husika. Hivyo idara imekuwa ikitoa masomo na mafundisha mbalimbali kwa njia ya softcopy kwa wale waliyoyahitaji masomo hayo.
10.  Idara inaendelea kushughulikia suala la usafiri hasa siku za ibada japo changamoto bado ni nyingi katika suala hili la usafiri.
11.  Idara imefanikiwa pia kufanya maintanince ya vyombo vya mawasiliano ikiwemo na utengenezaji wa tyres za generator.
KATIKA MALENGO MAREFU
Idara kwa kushirikiana na wakuu wengine wa idara imekuwa na kamati ikiwa chini ya mwenyekitii kwa ajili ya kushughulikia miradi mbalimbali tunayoendelea kuifatilia ili ianze kufanya kazi.

5. MAPATO NA MATUMIZI     
               5.1 MAPATO     
             Salio anzia…………………………………….220,900.00
            Makusanyo……………………...……..315,500.00  
              Usafirishaji P.A system……………….106, 500.00
             Picha za wahitimu 81@500……………..40,500.00
             Pesa ya uchakavu mkutano wa akina Mam…50,000.00
             Pesa ya uchakavu toka mahubiri ya zone(2013)..100,000.00
             Pesa ya uchakavu toka TU Retreat(2013)…50,000.00
             Pesa ya uchakavu toka Capital……………………………………………..20,000.00
             Pesa ya uchakavu katika harusi Dodoma kati...20,000.00
             Jumla ya mapato………………………702,500.00
                                                                                                 
            5.2 MATUMIZI YALIYOFANYIKA
              Gharama za Usafirishaji wa P.A System……45,000.00
              Usafirishaji wan nje toka Dom kati.……..….25, 000.00
              Matengenezo ya vifaa (ndani)………….…..380, 400.00
              Manunuzi ya  vitasa na kufuli………………………………………………..8,000.00
              Mawasiliano……...……………………..…2,500.00
              Editing passport size……………..…..……40,500.00
              Ushafirishaji wa PA System………………..80,000.00
              Matengenezo ya vifaa…………………..….70,000.00
              Ununuzi wa betri za microphone………..….2,500.00
             Jumla ya Matumizi yaliyofanyika…..….…653,900.00
            Salio ishia la Idara ya Mawasiliano.......... 269,500.00

 IDARA YA MAWASILIANO                                 
Salio anzia…..………………………........………….220, 900.00
Ongeza: Makusanyo…………………………….….702,500.00
                Jumla ya .……………………………..…923,400.00
Ondoa: Jumla ya Matumizi yaliyofanyika…….…653,900.00

Salio ishia la idara ya mawasiliano…………..…..269,500.00

6. CHANGAMOTO
Katika malengo yetu hatukuweza kufanikisha malengo yote kuyatendea kazi kutokana na sababu mbalimbali. kwa mfano hatukuweza kuongeza vifaa vyote kama ilivyo kwenye lengo letu la kwanza kutokana na ufinyu wa pesa tulizokusanya katika changizo la PA SYSTEM,
Pia hatujafanikiwa kubadilisha codi ya PA SYSTEM Kama ilivyokuwa imependekezwa katika lengo letu la tano kutokana na mafundi kutoeleweka.
Tatizo la usafiri bado ni changamoto katika idara hii kutoka na wanafunzi wenzetu kutotoa pesa zao mapema na kwa wakati hivyo tumekuwa tukilazimika wakati mwingine kutumia pesa zetu mifukoni ili kuwezesha suala nzima la usafiri.
Kumekuwa na tatizo kubwa la ubebaji wa vyombo vya mawasiliano hasa kwa wale wanaopangwa kutoonekana hivyo kutupatia wakati mgumu na mzigo mkubwa wana idara katika kuhakikisha vyombo vinafika mahali husika.
7. USHAURI
Tunapenda kuwaomba wanachama wenzetu kutupatia ushirikiano wa kutosha katika idara hii hasa katika ubebaji. Idara hii si ya Mapenzi, mwambenja, kazimoto, Dotto, Kibona au mtatilo. Tunahitaji msaada mkubwa kutoka kwa wanachama wenzetu katika kufanikisha idara hii. Tunawaomba sana.
Tunapenda pia kuwaomba wanachama wenzetu kutoa pesa za nauli mapema ikiwezekana kuanzia juma tatu na mwisho iwe ijumaa ili tujue idadi kamili ya watu na idadi ya magari tutakayoleta. Siku ya sabato hatutapokea pesa ya mtu yoyote Yule.

8. MAONI
Idara inapenda kuwasihi viongozi wapya wa TUCASA wanaoanza kazi yao kutopokea pesa za uchakavu mikononi mwao badala yake ziwekwe kwenye account na muhusika alete pay in slip kwa ajili ya kuandikishana mkataba.
 Viongozi wapya pia waendelee kufuatilia projector kutoka kwa vice president wetu pr. Geofrey Mbwana aliyoahidi kipindi cha retreat.
Tunapenda kuwaomba pia viongozi wapya kusimamia vyombo pasipo kuwa na muungiliano wa mtu yoyote asiyehusika katika idara hii ili kuondoa usumbufu katika kuoperate vyombo vya mawasiliano. Hivyo mtu yoyote asiyehusika katika idara hii tuwaachie wanaidara wenyewe wafanye kazi hiyo.
Tunawaomba pia wanaidara wenzetu wanaoingia kuendelea kuiboresha blogspot yetu zaidi ya hata pale tulipofanya sisi viongozi tunaomaliza mda wetu.
Pia tunawasihi wenzetu kuongeza vyombo vya mawasiliano ikiwemo 1 set of wireless microphone kwa ajili ya ufanisi wa ibada zetu.    
9. MWISHO
Idara inawashukuru sana wana TUCASA wote wa chuo kikuu cha Dodoma kwa namna tunavyoshirikiana katika kuimaliza kazi ya  bwana. MUNGU wetu wa Mbinguni na atubariki sana. Zaidi tunapenda kuomba ushirikiano wenu hadi hapo tutakapoimaliza kazi ya Bwana hapa duniani.

“LAKINI KATIKA MAMBO HAYO YOTE TUNASHIDA, NA ZAIDI YA                                   KUSHINDA, KWA YEYE ALIYETUPENDA.”
                                                          WARUMI 8:37
                                                    
         
                                               Imeandaliwa na
                                  IDARA YA MAWASILIANO
                        CHUO KIKUU CHA DODOMA (UDOM)
                                                2011/2013
                         

No comments:

Post a Comment