skip to main  |
      skip to sidebar
          
        
          
        
JE, WAJUA HISTORIA YA CHRISTMAS KWA UFUPI..??
 Biblia haijaweka wazi tarehe aliyozaliwa YESU. Historia inaonyesha wazi
 kuwa, tar 25/12 ni tarehe aliyozaliwa "Tammuz" ambaye wapagani 
waliamini kuwa Tammuz ni mungu wa mimea na mazao, hivyo basi wapagani 
waliazimisha kuzaliwa kwa Tammuz kila inapofika tarehe hiyo. Kanisa 
chini ya kiongozi Constantine likaamua kuingiza siku hii kama siku ya 
kuzaliwa YESU ili kuwavuta wapagani wajiunge na kanisa ili kuongeza 
mapato ya kodi. SWALI.. Je kuna uhusiano gani kati ya kuzaliwa kwa YESU 
na mti wa Christmas.??? Mti wa Christmas ni ishara ya kuzaliwa kwa 
Tammuz ambaye wapagani waliamini kuwa ndiye mungu wa mimea na mazao. 
HITIMISHO: Fanya Biblia pekee kuwa mwongozo wa maisha yako. KUMBUKA: 
Biblia ndiyo katiba ya kikristo. Acha kufuata mapokeo.
Imetupasa kumtii Mungu kuliko wanadamu. kama kuna fungu lolote linalosema Yesu alizaliwa tarehe 25/12 kwenye Biblia sema, na kama hakuna badilika kuanzia leo usiitukuze miungu ya babeli.
Mungu akubariki 
 
 
 
          
      
 
  
 
 
    
No comments:
Post a Comment